Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Tabia-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Tabia-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

6/22/2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Pili

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Pili


Mwenyezi Mungu alisema, Ingawaje kumwagwa kwa hasira ya Mungu ni dhana ya maonyesho ya tabia ya haki Yake, hasira ya Mungu kwa vyovyote vile haibagui walengwa wake au haina kanuni. Kinyume cha mambo ni kwamba, Mungu si mwepesi wa ghadhabu, wala Hakimbilii kufichua hasira Yake na adhama Yake. Aidha, hasira ya Mungu inadhibitiwa na kupimwa kwa kiwango fulani; hailinganishwi kamwe na namna ambavyo binadamu atakavyowaka kwa hasira kali au kutoa ghadhabu zake. Mazungumzo mengi kati ya binadamu na Mungu yamerekodiwa kwenye Biblia.

5/31/2019

Wimbo wa Kuabudu 126. Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee

Wimbo wa Kuabudu 126. Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee

I
Mungu huonyesha tabia Yake ya haki kupitia mbinu na kanuni za pekee,
haidhibitiwi na watu, matukio au vitu.
Na hakuna awezaye kubadili fikira au mawazo Yake,
au kumhimiza Atumie namna nyingine.
Hii ni asili ya pekee ya tabia ya haki ya Muumba!
Tabia Yake ya haki!

5/27/2019

Wimbo wa Kuabudu | 130. Mapenzi Ya Mungu Yamekuwa Wazi kwa Kila Mtu

Wimbo wa Kuabudu | 130. Mapenzi Ya Mungu Yamekuwa Wazi kwa Kila Mtu

Kutoka kwa uumbaji wa mwanadamu,
asili ya Mungu, mapenzi Yake, mali Yake na tabia
vimekuwa wazi kwa kila mmoja na wazi kwa wote.
I
Mungu hajawahi kamwe kuficha kiini Chake,
wala tabia ama mapenzi Yake kimakusudi.

5/11/2019

241. Mungu Huamua Mwisho wa Wanadamu Kutegemeza kwaKama Wanamiliki Ukweli

241. Mungu Huamua Mwisho wa Wanadamu Kutegemeza kwaKama Wanamiliki Ukweli

I
Ni wakati wa Mungu kuamua mwisho wa kila mtu,
si hatua ambapo Alianza kumfinyanga mwanadamu.
Mungu huandika katika kitabu Chake
kila neno na tendo la kila mtu.
Huviandika kimoja kimoja.
Mungu huamua hatima ya kila mtu
sio kutegemeza kwa kwa umri, cheo au mateso,
wala kiwango ambacho wao huvuta huruma,
lakini kulingana tu na kama wanao ukweli.

4/28/2019

96. Ni kwa Kumcha Mungu tu Ndiyo Uovu Unaweza Kuepwa

96. Ni kwa Kumcha Mungu tu Ndiyo Uovu Unaweza Kuepwa

Tabia ya Mungu ni adhimu na ya ghadhabu.
Yeye si mwanakondoo achinjwe na yeyote.
Yeye si karagosi, linalochezewa na yeyote anavyopenda.
Wala Yeye si hewa, inayoamriwa na watu pote.
Kama kweli unaamini kuweko kwa Mungu,
unapaswa kuwa na moyo unaomwogopa Mungu.

4/11/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 116

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 116

Kati ya maneno Yangu, mengi huwafanya watu kuhisi woga, mengi huwafanya watu watetemeke kwa hofu; bado mengine mengi sana huwafanya watu kuteseka na kukata tamaa, na bado mengine mengi husababisha uangamizaji wa watu. Wingi wa maneno Yangu, hakuna mtu anayeweza kuelewa au kufahamu vizuri. Ni wakati tu Ninapowaambia maneno Yangu na kuyafichua kwenu sentensi baada ya sentensi ndipo mnaweza kujua hali ya jumla; ukweli wa mambo maalum ya hakika, bado hamuelewi.

3/22/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 103

tabia ya Mungu,neno la Mungu,ukweli

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 103

Sauti ya mngurumo inatoka, ikiutetemesha ulimwengu mzima, ikiwahanikiza watu, na kuwafanya wachelewe kukwepa, na wengine wanauawa, baadhi wanaangamizwa, na wengine wanahukumiwa. Kweli ni kioja ambacho hakuna yeyote amewahi kukiona awali. Sikiliza kwa makini, milio ya radi inafuatana na sauti za kuomboleza, na sauti hii inatoka kuzimu, sauti hii inatoka jahanamu. Ni sauti yenye uchungu ya wale wana wa uasi ambao wamehukumiwa nami.

3/14/2019

Neno la Mungu | Onyo kwa Wale Wasioweka Ukweli katika Vitendo


Mwenyezi Mungu alisema, “Wale miongoni mwa ndugu na dada ambao daima hueneza ubaya wao ni vibaraka wa Shetani na hulivuruga kanisa. Watu hawa lazima siku moja wafukuzwe na kuondolewa. Katika Imani yao kwa Mungu, ikiwa watu hawana moyo wa kumcha Mungu ndani yao, ikiwa hawana moyo ambao ni mtiifu kwa Mungu, basi hawatashindwa tu kufanya kazi yoyote ya Mungu, lakini kinyume na hayo watakuwa watu wanaovuruga kazi ya Mungu na wanaomuasi Mungu.

3/07/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!


    Ninyi nyote mmeketi katika viti vya kifahari, mkiwafundisha wale wa vizazi vijana ambao ni wa aina yenu, ukiwafanya waketi nawe. Je, mngekosaje kujua kwamba wale “watoto” wenu walikuwa tayari hawana pumzi, na kwamba hawakuwa na kazi Yangu zamani? Utukufu Wangu huangaza kutoka nchi ya Mashariki hadi nchi ya Magharibi, lakini wakati utukufu Wangu huenea mpaka mwisho wa dunia na wakati unapoanza kuinuka na kuangaza, Nitaondoa utukufu wa Mashariki na kuuletea Magharibi ili kwamba watu hawa wa giza katika Mashariki ambao wameniacha Mimi watakuwa bila mwanga unaong’aa kuanzia hapo kwendelea.

3/06/2019

Neno la Mungu | Majani Yaangukayo Yatakaporudi kwa Mizizi Yake Utajuta Maovu Yote Ambayo Umefanya


Nyote mmeshuhudia wenyewe kazi ambayo Nimefanya miongoni mwenu, ninyi wenyewe mmesikia maneno ambayo Nimenena, nanyi mnajua mtazamo Wangu kuelekea kwenu, kwa hiyo mnapaswa kujua kwa nini Ninafanya kazi hii miongoni mwenu. Nitawaambia ukweli—ninyi ni vifaa tu vya kazi Yangu ya ushindi katika siku za mwisho; ninyi ni vyombo vya kupanua kazi Yangu miongoni mwa nchi za Mataifa. Mimi huzungumza kupitia kwa udhalimu wenu, uchafu wenu, upinzani na uasi wenu ili kupanua bora zaidi kazi Yangu ili jina Langu lienee miongoni mwa nchi za Mataifa, yaani, kuenea miongoni mwa nchi yoyote nje ya Israeli.

1/28/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I Sehemu ya Kwanza

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I Sehemu ya Kwanza

Leo tunawasiliana kuhusu mada muhimu. Hii ni mada ambayo imezungumziwa tangu kuanza kwa kazi ya Mungu mpaka sasa, na inayo umuhimu mkuu kwa kila mtu. Kwa maneno mengine, hili ni suala ambalo kila mmoja atakutana nalo kwenye mchakato wote wa kusadiki kwake katika Mungu na suala ambalo lazima lizungumziwe. Ni suala muhimu, lisiloepukika ambalo mwanadamu hawezi kujitenganisha nalo.

1/25/2019

Nyimbo za Dini | 13. Kama Tu Binadamu Watamwabudu Mungu wa Kweli Ndiyo Wataweza Kuwa na Jaala Nzuri

Mungu aliumba dunia hii. Aliumba binadamu.
Alikuwa mjenzi wa utamaduni wa zamani wa Ugiriki na ustaarabu wa binadamu.
Mungu tu ndiye Anayefariji, Anayefariji binadamu huyu.
Mungu pekee ndiye Anayejali kuhusu binadamu huyu mchana na usiku.
Kukua kwa binadamu na kuendelea 
hakutenganishwi na mamlaka ya Mungu, mamlaka kuu ya Mungu.
Historia na siku za baadaye za binadamu
zinahusiana sana na mpango wa Mungu, mpango wa Mungu.

1/12/2019

Wimbo wa Maneno ya Mungu | Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee

Wimbo wa Maneno ya Mungu Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee

I
Mungu huonyesha tabia Yake ya haki
kupitia mbinu na kanuni za kipekee,
haidhibitiwi na watu, matukio au vitu.
Na hakuna awezaye kubadili dhana au mawazo Yake,
au kumshawishi Ajaribu njia tofauti.
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba!
Tabia Yake ya haki!

1/04/2019

Wimbo wa Kuabudu ""Viumbe Wote Lazima Waje Chini ya Utawala wa Mungu"" | The Manifestation of the Power of God"

Wimbo wa Maneno ya Mungu Viumbe Wote Lazima Waje Chini ya Utawala wa Mungu

I
Mungu aliumba vitu vyote,
na hivyo Yeye hufanya viumbe vyote
kuja chini ya amri Yake, na kutii utawala Wake.
Anaamuru vitu vyote, akividhibiti katika mikono Yake.
Vitu hai, milima, mito na mwanadamu
lazima vyote vije chini ya amri Yake.

12/09/2018

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu"


Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu


Mwenyezi Mungu anasema, "Tabia ya mwanadamu lazima ibadilishwe kuanzia maarifa ya dutu yake na kupitia mabadiliko katika mawazo yake, asili, na mtazamo wa akili—kwa njia ya mabadiliko ya msingi. Ni kwa njia hii tu ndio mabadiliko ya kweli yatapatikana katika tabia ya mwanadamu.

10/31/2018

3. Jina la Mungu linaweza kubadilika, lakini asili Yake haitabadilika kamwe.

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu

3. Jina la Mungu linaweza kubadilika, lakini asili Yake haitabadilika kamwe.

Maneno Husika ya Mungu:
Kuna wale ambao wanasema kuwa Mungu habadiliki. Hiyo ni sahihi, lakini inaashiria mabadiliko ya tabia ya Mungu na pia kiini chake. Mabadiliko ya jina lake na kazi hayathibitishi ya kuwa kiini chake kimebadilika; kwa maneno mengine, Mungu siku zote Atakuwa Mungu, na hii kamwe haitabadilika.

8/26/2018

Swahili Worship Song "Unapoufungua Moyo Wako kwa Mungu" | Seeing the Love of God


Unapoufungua Moyo Wako kwa Mungu

Wakati hamumwelewi Mungu na hamjui asili Yake,
mioyo yenu haiwezi kamwe kufunguka, kufunguka kwa Mungu.
Mara utakapomwelewa Mungu wako,
utaelewa kile kilicho moyoni Mwake,
na kufurahia kile kilicho ndani Yake
kwa imani na usikivu wako wote.
Unapofurahia kile kilicho ndani ya moyo wa Mungu, kidogo kidogo,
siku baada ya siku,
unapofurahia kile kilicho ndani ya moyo wa Mungu,
moyo wako utakuwa wazi Kwake.

7/07/2018

Mwenyezi Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

Mwenyezi Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

Ndugu wawili wa kawaida, Beijing
Agosti 15, 2012
Julai 21, mwaka wa 2012 ilikuwa siku isiyosahaulika sana kwangu, pamoja na kuwa siku muhimu zaidi ya maisha yangu.
Siku hiyo, mvua kubwa ilikuwa ikinyesha katika Wilaya ya Fangshan jijini Beijing—ilikuwa kubwa kuliko yoyote iliyowahi kuonekana pale katika miaka sitini na mmoja. Muda mfupi baada ya saa 4 jioni, nilitoka nje mtaani ili kuangalia na nikaona kuwa maji yalikuwa kila mahali. Gari la familia yetu lilikuwa tayari limeelea, na sababu ya pekee gari hilo kutosombwa na mkondo wa maji ilikuwa kwamba lilizuiwa na kitu mbele yake kilicholizuia kusonga.

6/26/2018

Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

  Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?

Qingxin    Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan
Kuhusu kipengele cha ukweli cha "Mungu ni mwenye haki ", siku zote nilikuwa na ufahamu wa upuuzi kwa kiasi fulani. Nilidhani kuwa almradi mtu fulani hufichua upotovu katika kazi yake au hufanya makosa ambayo huiharibu kazi ya kanisa, mtu huyo atakabiliwa na rada, au kupoteza kazi yake au aathiriwe na adhabu. Hiyo ni haki ya Mungu. Kutokana na ufahamu huu usio sahihi, pamoja na hofu ya kupoteza kazi yangu kutokana na kufanya makosa katika kazi yangu, nilifikiria juu ya utaratibu "mjanja": Wakati wowote ninapofanya kitu vibaya, mimi hujaribu niwezavyo kutowaacha viongozi wajue kwanza, na kwa haraka kujaribu kukifidia mwenyewe na kufanya kila linalowezekana ili kukisawazisha.

5/23/2018

Ni Nini Ambacho Kimeidanganya Roho Yangu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

  Ni Nini Ambacho Kimeidanganya Roho Yangu?

Xu Lei     Mji wa Zaozhuang, Mkoa wa Shandong
Siku moja nilipokea taarifa juu ya mkutano. Kwa kawaida hili ni tukio la kufurahisha, lakini mara tu nilipofikiria jinsi kazi yangu hivi karibuni ilikuwa machafuko kabisa, sikuweza kujizuia kuhisi wasiwasi. Kama mkuu wangu angejua jinsi sikuwa nimemaliza kazi yoyote yangu, bila shaka angehitaji kunishughulikia, na huenda hata kunibadilisha na mwingine kazini. Ningefanya nini basi? Siku iliyofuata nilikwenda kwa mkutano na moyo mzito. Nilipofika huko, nikaona kwamba mkuu wangu alikuwa bado hajafika, lakini baadhi ya wafanyakazi wenzangu walikuwa hapo tayari. Niliwaza: "Sijui kazi yoyote yao iko katika hali gani.