Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ushuhuda-Kuipitia-Hukumu-Kristo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ushuhuda-Kuipitia-Hukumu-Kristo. Onyesha machapisho yote

10/07/2018

Ni Upendo wa Mungu Tu Ulio Halisi

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, wokovu

   Ni Upendo wa Mungu Tu Ulio Halisi

Xiaodong Mkoa wa Sichuan
Mungu alisema, “Taifa la China ambalo limepotoshwa kwa miaka elfu nyingi limeendelea mpaka leo. Kila aina ya virusi vinaendelea kutanuka na vinasambaa kila mahali kama tauni; kutazama tu mahusiano ya watu kunatosha kuona ni virusi vingapi viko ndani ya watu. Ni vigumu mno kwa Mungu kukuza kazi Yake katika sehemu kama hii iliyofungwa kikiki na kuambukizwa virusi.

9/28/2018

Mapambano ya Kufa na Kupona

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, neema

     Mapambano ya Kufa na Kupona

Chang Moyang Mjini Zhengzhou, Mkoani Henan
"Unapoutelekeza mwili, bila shaka kutakuwa na mapambano ndani. Shetani anataka ufuate dhana za mwili, kulinda maslahi ya mwili. Hata hivyo, neno la Mungu bado linakupa nuru na kukuangaza ndani, linakupa msukumo kwa ndani na kufanya kazi kutoka ndani. Katika hatua hii, ni juu yako kama unamfuata Mungu, au Shetani. Kila wakati ambapo ukweli unatendwa na kila wakati ambapo watu wanapofanya mazoezi ya kumpenda Mungu, kuna pambano kubwa.

9/22/2018

Kujijua kwa Hakika kwa Kuuelewa Ukweli Tu

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa

   Kujijua kwa Hakika kwa Kuuelewa Ukweli Tu

Wenwen Mji wa Changchun, Mkoa wa Jilin
Kwa maoni yangu, daima nililidhani kwamba mradi matendo ya nje yalionekana ya kufaa ambapo watu hawangeweza kuona upotovu wowote, basi lilichukuliwa kuwa mabadiliko. Kwa hiyo, nilizingatia kwa namna ya kipekee matendo ya nje katika kila kitu nilichokifanya. Nilijali tu kuhusu kama matendo yangu yalikuwa sahihi au la, na mradi tabia zangu za nje na matendo yalikuwa ya maana, nilikuwa sawa.

9/13/2018

Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, upendo wa Mungu

   Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki

Chen Lu Wilaya ya Tonglu, Mkoa wa Zhejiang
Nilizaliwa miaka ya 1980 katika kijiji—tulikuwa tumekuwa familia ya wakulima kwa vizazi vingi. Nilijiingiza katika masomo yangu ili niweze kuhitimu kuingia katika chuo na kuepuka maisha ya kijijini ya umasikini na hali ya kuwa nyuma. Nilipoanza shule ya upili, nilikutana na Historia ya Sanaa ya Magharibi, na wakati nilipoona picha nyingi za kupendeza kama vile "Mwanzo," "Bustani ya Edeni," na "Mlo wa Mwisho," ni hapo tu nilipojua kwamba kulikuwa na Mungu katika ulimwengu aliyeumba vitu vyote.

9/10/2018

Utajiri wa Maisha

      Utajiri wa Maisha

Wang Jun Mkoa wa Shandong
Kwa miaka mingi tangu kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, mke wangu na mimi tumepitia hili pamoja chini ya ukandamizaji wa joka kubwa jekundu. Katika wakati huu, ingawa nimekuwa na udhaifu, maumivu, na machozi, nahisi kwamba nimenufaika pakubwa kutoka kwa uzoefu wa ukandamizaji huu. Uzoefu huu mchungu haujanifanya tu kuona kwa dhahiri asili mbovu ya kupinga maendeleo, na sura mbaya ya joka kubwa jekundu, lakini pia nimetambua asili yangu mwenyewe ya upotovu.

9/07/2018

Mabadiliko ya Kweli Humaanisha Nini?

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, upendo wa Mungu

   Mabadiliko ya Kweli Humaanisha Nini?

Jinru    Mji wa Nanyang, Mkoa wa Henan
Wakati ndugu wa kiume au wa kike alipoonyesha dosari zangu au hakusikiza kauli yangu ama sikuhisi kushawishika au nilibishana nao. Nilijutia vitendo vyangu baadaye, lakini nilipokabiliwa na mambo haya, sikuweza kujizuia mwenyewe kuifichua tabia yangu potovu. Nilisumbuliwa na hili kwa kina, na nikafikiri: Kwa nini maneno ya wengine yanaweza kuniaibisha hadi kukasirika? Na kwa nini sijabadilika hata kidogo licha ya miaka minane ya kumfuata Mungu? Nilikuwa na wasiwasi na tena na tena nilimtafuta Mungu kwa jibu.

9/01/2018

Kupitia kwa Majonzi Makuu, Nimevuna Faida Kubwa

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ushuhuda

  Watu Wasio na Hila Sio Lazima Wawe Waaminifu

Rongguang   Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan
Baada ya kumfuata Mwenyezi Mungu, niliwekwa katika jela kwa sababu mimi niliamini katika Mungu. Wakati huo nilikuwa muumini mpya na Mungu alikuwa amenipa nguvu ili niweze shikilia msimamo katika ushahidi wangu. Hata hivyo, niliamini kimakosa kuwa nilikuwa na kimo; nilidhani kwamba nilikuwa na kiasi kikubwa cha imani, upendo na uaminifu kwa Mungu, kwa hiyo sikuzingatia hasa kula na kunywa maneno ya Mungu ya hukumu na kuadibu.

8/31/2018

Watu Wasio na Hila Sio Lazima Wawe Waaminifu

  Watu Wasio na Hila Sio Lazima Wawe Waaminifu

Cheng Mingjie    Jiji la Xi'an, Mkoa wa Shaanxi
Mimi hujiona kuwa mtu wa aina ya kuwa wazi na mchangamfu. Mimi huzungumza na watu kwa njia ya waziwazi; chochote ninachotaka kusema, mimi husema—mimi sio aina ya mtu wa kuzungukazunguka. Katika kuingiliana kwangu na watu mimi huwa ni mwaminifu na wazi kiasi. Mara kwa mara, mimi hudanganywa na kudhihakiwa kwa sababu ya kuwaamini wengine kwa urahisi. Ilikuwa tu baada ya kuanza kwenda kanisani nilipopata mahali ambapo ningepaita pangu.

8/28/2018

Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, maombi

   Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

Tong Xin    Mkoa wa Fujian
Nilizaliwa vijijini. Nilitoka kwa nasaba ya wakulima wanyenyekevu na zaidi ya hayo familia yetu ilikuwa na watu wachache, kwa hiyo mara nyingi tulikuwa tunadhulumiwa. Nilipokuwa na umri wa miaka 13, kulikuwa na mtoto aliyepigwa na mtu fulani kutoka nje ya kijiji chetu. Wanakijiji walimlaumu kwa uongo baba yangu kwa kuchochea hilo na wakasema walitaka kupekua nyumba yetu na kuchukua ngawira mali yetu, kuchukua nguruwe wetu na hata kumpiga baba yangu.

8/25/2018

Nilifurahia karamu kubwa

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, maombi

   Nilifurahia karamu kubwa

Xinwei    Mkoa wa Zhejiang
Juni 25 na 26 zilikuwa siku zisizohaulika. Eneo letu la Zhejiang lilipata tukio kubwa, viongozi wengi na wafanyakazi wa eneo wakiwa wamekamatwa na joka kubwa jekundu. Ni wachache wetu tu tuliokimbia bila kuumia na, mioyo yetu ikiwa imejaa shukrani, tulikula kiapo cha siri kwa Mungu: kushirikiana vizuri na kazi iliyokuwa ifuate. Kufuatia hilo tulianza kazi yenye msisimko na shughuli nyingi ya kushughulika na matokeo.

8/23/2018

Umuhimu wa Uratibu Katika Huduma

    Umuhimu wa Uratibu Katika Huduma

Mei Jie    Jijini Jinan, Mkoani Shandong
Baada ya kubadilisha uongozi wa kanisa kurudi kwa ule wa asili, ubia uliwekwa kwa kila ngazi ya kiongozi katika nyumba ya Mungu. Wakati huo, nilifikiri kwamba huu ulikuwa mpangilio mzuri. Nilikuwa wa ubora wa tabia wa chini na nilikuwa na kazi nyingi; kwa kweli nilihitaji mbia wa kunisaidia kukamilisha kila aina ya kazi katika eneo langu.

8/20/2018

Niliona Kimo Changu cha Kweli kwa Dhahiri

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ukweli

  Niliona Kimo Changu cha Kweli kwa Dhahiri

Ding Xiang    Jijini Tengzhou, Mkoa wa Shandong
Katika mkutano wa viongozi wa kanisa niliowahi kuhudhuria, kiongozi wa kanisa aliyekuwa amechaguliwa hivi karibuni alisema: “Sina kimo cha kutosha. Mimi ninahisi sifai kuutimiza wajibu huu. Mimi ninahisi kushinikizwa na vitu vingi sana, kwa kiwango kwamba mimi sijaweza kupata usingizi kwa siku na usiku kadhaa mtawalia....” Wakati huo, mimi nilikuwa nimebeba mizigo katika kumfuatilia Mungu, kwa hivyo niliwasiliana naye: “Kazi zote hufanywa na Mungu; mwanadamu hushirikiana kidogo tu.

8/19/2018

Ni Muhimu Sana Kutii Kazi ya Roho Mtakatifu

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, maombi

 Ni Muhimu Sana Kutii Kazi ya Roho Mtakatifu

Xiaowei    Mji wa Shanghai
Wakati fulani kitambo, hata kama daima nilipata msukumo kiasi na fadhila wakati dada mmoja aliyeshiriki nami alishiriki nuru aliyokuwa amepata wakati alipokula na kunywa neno la Mungu, pia kila wakati nilikuwa na hisia ya muda mrefu kuwa alikuwa anajionyesha. Ningejiuliza, “Nikimjibu sasa hivi, sitakuwa nikimtia moyo? Kwa namna hiyo, sitaonekana basi kuwa duni kumliko yeye?” Matokeo yake yakawa, nilikataa kutaja maoni yangu mwenyewe katika ushirika au kutoa maoni kuhusu mawazo yoyote aliyoshirikisha.

6/28/2018

Hakuna Utendewaji Maalum katika Kanisa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

   Hakuna Utendewaji Maalum katika Kanisa

Liu Xin     Mji wa Liaocheng, Mkoa wa Shandong
Baada ya kumfuata Mungu kwa miaka hii, nilihisi kuwa nilikuwa nimevumilia mateso na kulipa gharama fulani, kwa hiyo nilianza kuyategemea mapato yangu ya zamani na kuringia ukubwa wangu. Niliwaza: Nimeondoka nyumbani kwa miaka mingi na familia yangu haijaisikia kutoka kwangu kwa muda mrefu. Katika hali hii, kanisa hakika litanitunza. Hata nisipofanya kazi yangu vizuri hawatanituma nyumbani. Si zaidi ya hayo wataniondoa tu na kunielekeza kufanya kazi nyingine. Kutokana na kufikiri kama huko, sikuwa na mzigo wowote kamwe katika kazi yangu. Nilipuuza kila kitu, na hata nikaiona kazi ya injili kama mzigo, daima nikiishi katika matatizo na visingizio.

6/27/2018

Kuelewa Mapenzi ya Mungu Katikati ya Matatizo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Injili

 Kuelewa Mapenzi ya Mungu Katikati ya Matatizo

Xiao Rui    Mji wa Panzhihua, Mkoa wa Sichuan
Nilipokuwa nikihubiri injili nilikutana na viongozi wa madhehebu ambao walisema uongo ili kupinga na kuvuruga, na kuwaita polisi. Hili lilisababisha wale niliokuwa nikihubiria kutothubutu kuwasiliana nasi, na wale ambao walikuwa tu wameikubali injili kutoweza kuwa na imani katika kazi ya Mungu. Nilipofanya kazi kwa bidii sana lakini matokeo yalikuwa duni, nilifikiri: kazi ya Kiinjili ni ngumu sana kutekeleza. Lingekuwa jambo la kustaajabisha sana kama Mungu angeonyesha miujiza kiasi na kuwaadhibu wale ambao husema uongo pamoja na wale ambao kwa uzito kabisa humpinga Mungu kuwaonyesha wale ambao wamedanganywa.

6/26/2018

Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

  Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?

Qingxin    Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan
Kuhusu kipengele cha ukweli cha "Mungu ni mwenye haki ", siku zote nilikuwa na ufahamu wa upuuzi kwa kiasi fulani. Nilidhani kuwa almradi mtu fulani hufichua upotovu katika kazi yake au hufanya makosa ambayo huiharibu kazi ya kanisa, mtu huyo atakabiliwa na rada, au kupoteza kazi yake au aathiriwe na adhabu. Hiyo ni haki ya Mungu. Kutokana na ufahamu huu usio sahihi, pamoja na hofu ya kupoteza kazi yangu kutokana na kufanya makosa katika kazi yangu, nilifikiria juu ya utaratibu "mjanja": Wakati wowote ninapofanya kitu vibaya, mimi hujaribu niwezavyo kutowaacha viongozi wajue kwanza, na kwa haraka kujaribu kukifidia mwenyewe na kufanya kila linalowezekana ili kukisawazisha.

6/24/2018

Upendo wa Wokovu wa Mungu kwa Wanadamu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, maombi

  Upendo wa Wokovu wa Mungu kwa Wanadamu

Danyi     Mkoa wa Sichuan
Kuna hisia ya hatia ambayo huchemka moyoni mwangu kila wakati ninapoona maneno haya ya Mungu: “Tatizo kubwa mno kwa mwanadamu ni kuwa yeye hufikiria tu kuhusu hatima yake na matarajio, na kuyaabudu. Mwanadamu humfuata Mungu kwa ajili ya hatima yake na matarajio; yeye hamwabudu Mungu kwa sababu ya upendo wake kwake. Na kwa hivyo, katika ushindi kwa mwanadamu, ubinafsi wa mwanadamu, uroho na vitu ambavyo sana sana huzuia ibada yake kwa Mungu ni sharti viondolewe.

6/23/2018

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, maombi

   Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Momo     Mji wa Hefei, Mkoa wa Anhui
Kabla ya kumwamini Mungu, bila kujali chochote nilichokuwa nikifanya, sikuwahi kutaka kubaki nyuma. Nilikuwa tayari kukubali shida yoyote ili mradi ingemaanisha ningeinuka juu ya kila mtu mwingine zaidi. Baada ya kumkubali Mungu, mtazamo wangu uliendelea kuwa sawa, kwa sababu niliamini kikamilifu msemo, "Hakuna maumivu, hakuna faida," na kuona mtazamo wangu kama ushahidi wa msukumo wangu. Wakati Mungu alinifichulia ukweli, hatimaye niligundua kuwa nilikuwa nikiishi chini ya jozi la Shetani, nikiishi chini ya miliki yake.

6/22/2018

Uzoefu wa Kutenda Ukweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ushuhuda

   Uzoefu wa Kutenda Ukweli

Hengxin     Jiji la Zhuzhou, Mkoa wa Hunan
Sio muda mrefu mno uliopita, nilisikia "Ushirika na Kuhubiri Kuhusu Kuingia kwa Maisha," jambo ambalo lilinielekeza kuelewa kwamba ni wale tu wanaotenda ukweli wanaoweza kupata ukweli na hatimaye kuwa wale ambao wanaomiliki ukweli na ubinadamu hivyo kupata kibali cha Mungu. Kuanzia hapo kwendelea, kwa makusudi nilifanya jitihada za kuunyima mwili wangu na kutenda ukweli katika maisha yangu ya kila siku. Wakati fulani baadaye, nilitambua kwa furaha kwamba ningeweza kutenda ukweli kiasi. Kwa mfano, siku za nyuma niliogopa kuonyesha upande wangu mwovu kwa wengine.

6/21/2018

Kupitia Upendo Maalum wa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

   Kupitia Upendo Maalum wa Mungu

Jiayi     Mji wa Fuyang, Mkoa wa Anhui
Asili yangu ni ya kiburi hasa; bila kujali ninafanya nini, mimi daima hutumia werevu na ujuzi wa kubuni ili kuonyesha akili yangu na kwa hiyo mara kwa mara hukiuka mipango ya kazi ili nifanye mambo kwa njia yangu mwenyewe. Mimi ni mwenye kiburi hasa kuhusu kuchagua watu kwa cheo fulani. Ninaamini kuwa nina talanta ya kipekee na umaizi ambavyo hunisaidia daima kumchagua mtu sahihi. Kwa sababu ya hili, nilipomchagua mtu, singechunguza kwa dhati ili kuelewa hali zote za mtu niliyetaka kumchagua.