Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo makusudi-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo makusudi-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

5/26/2019

Wimbo wa Kuabudu | 249. Je, Umehisi Matumaini ya Mungu Kwako?

Wimbo wa Kuabudu | 249. Je, Umehisi Matumaini ya Mungu Kwako?

I
Ni nani aliyetafutwa na Mungu katika ulimwengu huu usio na mwisho?
Ni nani ambaye amesikia mwenyewe maneno ya Roho wa Mungu?
Nani kati yenu anayeweza kumjibu Ayubu? Ni nani kati yenu ni Petro?
Kwa nini Mungu amemtaja Ayubu na Petro mara nyingi?
Je, umeelewa matumaini ya Mungu kwako?
Eh, unapaswa kutumia muda mwingi kutafakari, eh, kutafakari.

3/15/2019

Neno la Mungu | Sura ya 97

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,neema

Neno la Mungu | Sura ya 97

Mwenyezi Mungu alisema, Nitafanya kila mtu aone matendo Yangu ya ajabu na kusikia maneno Yangu ya hekima. Ni lazima iwe kila mtu na ni lazima iwe juu ya kila suala. Hii ni amri Yangu ya utawala na ni ghadhabu Yangu. Nitahusisha kila mtu na kila jambo ili watu wote kutoka mwisho mmoja wa ulimwengu hadi mwingine wataona kwa macho yao wenyewe, la sivyo Sitaacha kamwe. Ghadhabu Yangu imemwagwa kikamilifu na hakuna hata chembe imezuiwa. Inaelekezwa kwa kila mtu mmoja ambaye anakubali jina hili (hivi karibuni itageuzwa juu ya mataifa yote ya dunia).

3/04/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (9)


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (9)


Tamaduni za asili na mitazamo ya kiakili madhubuti vimeweka kivuli katika roho safi na ya kitoto ya mwanadamu, vimeshambulia roho ya mwanadamu bila ubinadamu hata kidogo kana kwamba anaondolewa hisia na hali yoyote ya nafsi. Mbinu za mashetani hawa ni za kikatili kupita kiasi, na ni kana kwamba "elimu" na "malezi" vimekuwa ni njia za kitamaduni ambazo kwazo mfalme wa mashetani anamchinja mwanadamu; kwa kutumia "mafundisho yake ya kina" anafunika kabisa roho yake mbaya, akivaa mavazi ya kondoo ili kupata imani ya mwanadamu na halafu kusubiri mwanadamu akiwa amelala na kummeza kabisa.

2/19/2019

Neno la Mungu | Sisitiza Uhalisi Zaidi

Neno la Mungu | Sisitiza Uhalisi Zaidi


Kila mtu ana uwezekano wa kukamilishwa na Mungu, kwa hiyo kila mtu anapaswa kuelewa ni huduma gani kwa Mungu inayofaa zaidi makusudi ya Mungu. Watu wengi hawajui kumwamini Mungu humaanisha nini na hawajui kwa nini wanapaswa kumwamini Mungu. Yaani, watu wengi zaidi hawana ufahamu wa kazi ya Mungu au lengo la mpango wa usimamizi wa Mungu. Hadi leo, watu wengi zaidi bado wanadhani kumwamini Mungu kunahusu kwenda mbinguni na roho zao kuokolewa.

1/29/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I Sehemu ya Pili

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I Sehemu ya Pili

Ili kuelewa tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe lazima muanzie na jambo dogo sana. Jambo hilo dogo sana mnalopaswa kuanzia ni nini? Kwanza kabisa, Nimezikusanya baadhi ya sura kutoka kwenye Biblia. Taarifa iliyo hapa chini inayo mistari ya Biblia, ambayo yote inahusiana na mada ya tabia ya Mungu, kazi ya Mungu na Mungu Mwenyewe.

8/12/2018

Ufafanuzi wa Tamko la Thelathini na Tano

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu

Siku hizi, binadamu wote, kwa viwango vinavyotofautiana, wameingia katika hali ya kuadibu. Kama tu alivyosema Mungu“Naenda mbele na binadamu sako kwa bako.” Hii ni kweli kabisa, lakini watu bado hawawezi kulielewa kabisa wazo hili. Kutokana na hili, sehemu ya kazi ambayo wamefanya imekuwa si lazima. Mungu alisema, “Mimi husaidia na kuwaruzuku kwa mujibu wa kimo chao.

5/30/2018

Kusudi la Kazi ya Usimamizi ya Mungu ni Kumwokoa Binadamu


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa



Kusudi la Kazi ya Usimamizi ya Mungu ni Kumwokoa Binadamu

Upendo na huruma za Mungu
hupenyeza kazi Yake
ya usimamizi kwa utondoti.
I
Ikiwa mwanadamu ahisi mapenzi Yake ya huruma au la,
Yeye hachoki kufuatilia kazi Anayohitaji kufanya.
Ikiwa mwanadamu aelewa usimamizi Wake au la,
kazi Yake huleta usaidizi na utoaji unaoweza kuhisiwa na wote.
Upendo na huruma za Mungu
hupenyeza kazi Yake
ya usimamizi kwa utondoti.

5/09/2018

Umeme wa Mashariki | Kuvunja Pingu

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, upendo wa Mungu

   Umeme wa Mashariki | Kuvunja Pingu

Zhenxi Jijini Zhenzhou, Mkoani Hena
Miaka kumi iliyopita, nikiendeshwa na asili yangu ya kiburi, sikuweza kamwe kutii kikamilifu mipangilio ya kanisa. Ningetii ikiwa ilinifaa, lakini iwapo haingenifaa ningechagua iwapo ningetii au la. Hili lilisababisha kukiuka sana mipangilio ya kazi wakati wa kutimiza wajibu wangu. Nilifanya jambo langu mwenyewe na kuichukiza tabia ya Mungu, na hivyo baada ya hapo nilitumwa nyumbani. Baada ya miaka kadhaa ya kujitafakari, nilikuwa kwa kiwango fulani na maarifa ya asili yangu mwenyewe, lakini kuhusu kipengele cha ukweli ambacho ni kiini cha Mungu bado sikuwa na maarifa mengi. Baadaye, kanisa lilinipa nafasi nyingine, lakini nilipokuwa nikisimamia kazi ya injili, nilianza kuwa na shaka kumhusu Mungu: Mimi ni mpotovu sana na pia nilikuwa nimeichukiza tabia ya Mungu.

4/11/2018

Umeme wa Mashariki | Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa

Umeme wa Mashariki,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Kanisa

     Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa

Xinyi Mji wa Xi’an, Mkoa wa Shaanxi
Katika ziara zangu za karibuni kwa makanisa, mara nyingi niliwasikia viongozi na wafanyakazi wakisema kwamba watu wengine, baada ya kuhudhuria ushirika na mimi, waligeuka hasi, wanyonge na walikosa motisha ya kuendelea kutafuta. Wengine walisema ilikuwa vigumu sana kumwamini Mungu na walimwelewa Mungu visivyo. Wengine walisema kwamba hali zao zilikuwa nzuri kabla ya wao kukutana na mimi, lakini punde tu waliponiona, walihisi shinikizo kubwa mno na wasio na raha. ...Niliposikia haya yote, nilihuzunika, na nilihisi kukosewa vibaya—kila wakati nilipokuja kushiriki na wao ningeishi kwa baadhi ya siku, na, ili kutatua shida zao, nilipitia na kudondoa kama mifano vifungu vingi vya neno la Mungu, nikizungumza hadi nilipokauka mdomo, na wakati huo wote nikifikiri kwamba juhudi zangu zilikuwa zimetoa matokeo mazuri.