Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Paulo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Paulo. Onyesha machapisho yote

12/30/2017

Sura ya 38. Yeye Ambaye Hukosa Ukweli Hawezi Kuwaongoza Wengine

Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu,Kanisa la Mwenyezi Mungu

Umeme-wa-Mashariki-Kumbukumbu-za-Maongezi-ya-Kristo

Sura ya 38. Yeye Ambaye Hukosa Ukweli Hawezi Kuwaongoza Wengine

Mwenyezi Mungu alisema, Je, kweli mnaelewa kuhusu mabadiliko katika tabia ya mtu? Mabadiliko katika tabia yanamaanisha nini? Je, mnaweza kutambua mabadiliko katika tabia? Ni hali zipi zinaweza kufikiriwa kuwa mabadiliko katika tabia ya maisha ya mtu, na ni hali zipi ambazo ni mabadiliko tu katika tabia ya nje? Tofauti ni ipi kati ya mabadiliko katika tabia ya mtu ya nje na mabadiliko katika maisha ya mtu ya ndani?

12/28/2017

Sura ya 36. Kujijua Mwenyewe Hasa Ni Kujua Asili ya Binadamu | Umeme wa Mashariki

Mwenyezi Mungu alisema, La muhimu katika kufikia badiliko la tabia ni kujua asili ya mtu mwenyewe, na hili ni lazima litoke kwa ufunuo na Mungu. Ni katika neno la Mungu tu ambapo mtu anaweza kujua asili yake ya kutia kinyaa, afahamu katika asili yake mwenyewe sumu mbalimbali za Shetani, atambue kuwa yeye ni mjinga na mpumbavu, na atambue dalili dhaifu na hasi katika asili yake mwenyewe. Mara haya yanapojulikana kikamilifu, na unaweza kwa hakika kunyima mwili, daima kutekeleza neno la Mungu, na kuwa na mapenzi ya kujiwasilisha kikamilifu kwa Roho Mtakatifu na kwa neno la Mungu, basi umeianza njia ya Petro. Bila neema ya Mungu, kama hakuna kupata nuru na mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu, ingekuwa vigumu sana kuitembea njia hii, kwa sababu watu hawana ukweli na hawawezi kujisaliti wenyewe.

10/20/2017

Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea

Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu, Kanisa la Mwenyezi Mungu
Watu wengi wanamwamini Mungu kwa ajili ya hatima yao ya baadaye au kwa ajili ya starehe ya muda mfupi. Kwa wale ambao hawajapitia ushughulikiaji wowote, imani kwa Mungu ni kwa ajili ya kuingia mbinguni, ili kupata tuzo. Sio ili kufanywa wawe na ukamilifu, au kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu. Ambayo ni kusema kwamba watu wengi hawamwamini Mungu ili watimize majukumu yao, au kukamilisha wajibu wao.