Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo uaminifu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo uaminifu. Onyesha machapisho yote

4/22/2019

Nyimbo za kusifu | 237. Kile Vijana Hawana Budi Kufuatilia

Nyimbo za kusifu | 237. Kile Vijana Hawana Budi Kufuatilia

I

Macho yanayochukiza na udanganyifu

sivyo wanavyofaa kuvimiliki vijana.

Njia za kuogofya na haribifu

sizo wanazofaa kuzitenda vijana.

Wanafaa kuwa na malengo,

kwa shauku wajitahidi kuendelea,

sio kukata tamaa juu ya matarajio yao,

wadumishe imani katika maisha, katika wakati ujao.

2/10/2018

Umeme wa Mashariki | Kutambua Kuwa Nimekuwa Nikiitembea Njia ya Mafarisayo

Umeme wa Mashariki,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Biblia

Mafarisayo

 

Kutambua Kuwa Nimekuwa Nikiitembea Njia ya Mafarisayo

Wuxin Mji wa Taiyuan, Mkoa wa Shanxi
Kitu ambacho tumezungumzia mara kwa mara katika ushirikiano wa awali ni njia ambazo zilitembewa na Petro na Paulo. Inasemekana kwamba Petro alizingatia kujijua mwenyewe na kumjua Mungu, na alikuwa mtu ambaye Mungu alimpenda, ilhali Paulo alizingatia tu kazi yake, sifa na hadhi yake, na alikuwa mtu ambaye Mungu alimdharau. Daima nimekuwa na hofu ya kuitembea njia ya Paulo, ambayo ndiyo sababu mimi kwa kawaida mara nyingi husoma maneno ya Mungu kuhusu uzoefu wa Petro ili kuona jinsi alivyopata kumjua Mungu. Baada ya kuishi hivi kwa muda, nilihisi kwamba nilikwishakuwa mtiifu zaidi kuliko hapo awali, hamu yangu ya sifa na hadhi ilikuwa imedidimia, na kwamba nilikuwa nimepata kujijua kidogo.

1/23/2018

Swahili Christian Musical Drama "Hadithi ya Xiaozhen" | Mungu ni upendo


Christian Music Video Swahili “Hadithi ya Xiaozhen” | Mungu ni upendo

Xiaozhen alikuwa Mkristo mwenye moyo safi, ulio na huruma, ambaye kila wakati alikuwa akiwashughulikia wenzake kwa uaminifu. Hata hivyo, ilipokuwa ni kwa manufaa yao, marafiki wake wa awali waligeuka na kuwa maadui wake. Baada ya kuteseka kutokana na msiba huu, Xiaozhen alilazimika kuuacha moyo wake wa kweli na kanuni zake za awali. Alianza kuisaliti dhamiri yake mwenyewe iliyo nzuri na roho safi, na kugaagaa katika kinamasi cha ulimwengu mbaya. … Huku akianguka kutoka kwa rehema na kutembea katika njia ya upotovu, alikanyagwa na ulimwengu na kukung’utwa na makovu na vilio.

12/05/2017

Umeme wa Mashariki | Wewe U Mwaminifu kwa Nani?

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, maombi
Mwenyezi Mungu alisema, Kila siku mnayoiishi sasa ni ya maana sana na muhimu sana kwa hatima yenu na majaliwa yenu, kwa hivyo mnapaswa kufurahia kila mlicho nacho na kila dakika inayopita. Mnapaswa kutumia muda wenu vizuri ili muweze kujinufaisha, ili msije kuishi maisha haya bure. Pengine mnajihisi kukanganyikiwa mnaojiuliza ni kwa nini Ninazungumza maneno haya.