XII. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Wanawali Wenye Busara Wakiisikia Sauti ya Mungu
3. Kuna tofauti ipi kati ya maneno ya Mungu yaliyowasilishwa na manabii katika Enzi ya Sheria na maneno ya Mungu yaliyoonyeshwa na Mungu mwenye mwili?
Maneno Husika ya Mungu:
Katika Enzi ya Neema, Yesu pia Alinena mengi na kufanya kazi nyingi. Alikuwaje tofauti na Isaya? Alikuwaje tofauti na Danieli? Je, Alikuwa nabii? Ni kwa nini inasemekana kwamba Yeye ni Kristo? Kuna tofauti gani baina yao? Wote walikuwa wanadamu walionena maneno, na maneno yao yalionekana sawa kwa wanadamu. Wote walinena na kufanya kazi.