Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Dondoo-za-Video. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Dondoo-za-Video. Onyesha machapisho yote

12/05/2018

Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (5) - Ni Mahali Gani Ambapo Bwana Ametutayarishia?


Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (5) - Ni Mahali Gani Ambapo Bwana Ametutayarishia?

Miaka elfu mbili iliyopita, Bwana Yesu aliahidi, "Naenda kuwatayarishia mahali. Na nikienda kuwatayarishia mahali, nitarudi tena na kuwapokea kwangu; ili mahali nipo, muweze kuwa pia" (Yohana 14:2-3).

12/01/2018

Filamu za Kikristo "Kumbukumbu Chungu" | Unamfahamu Paulo kwa Kweli?


Filamu za Kikristo "Kumbukumbu Chungu" | Unamfahamu Paulo kwa Kweli?

Kwa miaka elfu mbili, Paulo amekuwa kielelezo cha kufuatwa kwa wale wote wanaomsadiki Bwana. Lakini tunamfahamu Paulo kwa kweli? Tunajua kwa kweli ukweli wa Paulo uliofichwa wa yeye kufanya kazi kwa uangalifu na bidii nyingi kwa ajili ya Bwana? Asili ya Paulo ni ipi, na kiini chake ni kipi? Video hii fupi itatusaidia kumfahamu Paulo halisi!

11/23/2018

"Jina la Mungu Limebadilika?!" (1) - Je, Kuna Maneno Mengine ya Mungu Kando ya Yale Yaliyo kwenye Biblia?


"Jina la Mungu Limebadilika?!" (1) - Je, Kuna Maneno Mengine ya Mungu Kando ya Yale Yaliyo kwenye Biblia?

Biblia inasema, "Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kilichofungwa kwa mihuri saba" (Ufunuo 5:1). "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno ambalo Roho aliyaambia makanisa; Kwa yule ashindaye nitampa mana iliyofichwa aile" (Ufunuo 2:17).

11/20/2018

Filamu za Kikristo "Kumbukumbu Chungu" | Ni Vigezo Vipi vya Kuingia Kwenye Ufalme wa Mbinguni?


Filamu za Kikristo "Kumbukumbu Chungu" | Ni Vigezo Vipi vya Kuingia Kwenye Ufalme wa Mbinguni?

Kuhusiana na ni mtu aina gani anayeweza kuingia kwenye ufalme wa mbinguni, Bwana Yesu alisema, "ila yule atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni" (Mathayo 7:21). Kwa hivyo ni mtu aina gani hasa anayefanya mapenzi ya Baba wa mbinguni? Watu wengi husadiki kwamba wale wanaofuata mfano wa Paulo na kufanya kazi kwa uangalifu na bidii nyingi kwa ajili ya Bwana ndio wanaofanya mapenzi ya Baba wa mbinguni.

11/17/2018

Filamu za Kikristo "Kumbukumbu Chungu" | Nini Hasa Ni Uhusiano Kati ya Kuokolewa na Kuingia kwenye Ufalme wa Mbinguni?


Filamu za Kikristo "Kumbukumbu Chungu" | Nini Hasa Ni Uhusiano Kati ya Kuokolewa na Kuingia kwenye Ufalme wa Mbinguni?

Watu wengi wanasadiki kwamba kwa kumsadiki Bwana Yesu dhambi zao zinasamehewa, kwamba wanaokolewa kupitia kwa imani, na zaidi kwamba pindi mtu anapookolewa anaokolewa milele, na pindi Bwana anaporudi ananyakuliwa na kuingia kwenye ufalme wa mbinguni!

11/14/2018

Filamu za Injili | “Kumbukumbu Chungu” Movie Clip: Wokovu Kupitia Imani Pekee Unaweza Kuwa Tiketi ya Kuingia Katika Ufalme wa Mbinguni?

Filamu za Injili | “Kumbukumbu Chungu” Movie Clip: Wokovu Kupitia Imani Pekee Unaweza Kuwa Tiketi ya Kuingia Katika Ufalme wa Mbinguni?



Hasa ni mtu aina gani anayeweza kuingia kwenye ufalme wa mbinguni? Baadhi ya watu hufikiria dhambi zetu zinasamehewa pindi tunaposadiki Bwana, kwamba pindi tunapookolewa basi tunaokolewa milele, na kwamba mtu aina hii anaweza kunyakuliwa na kuingia kwenye ufalme wa mbinguni.

11/08/2018

Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Je, Kuamini katika Biblia Kunaweza Kuwakilisha Kumwamini Mungu?


Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Je, Kuamini katika Biblia Kunaweza Kuwakilisha Kumwamini Mungu?

Wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini hushikilia maneno ya Paulo katika Biblia yanayosema "Maandiko yote yametolewa kwa msukumo wa Mungu," wakiamini kwamba Biblia ni maneno ya Mungu kabisa na kufanya yote wanayoweza kuiinua Biblia na kuishuhudia, na kuifanya Biblia na Mungu kuwa visawe. Wanaamini kwamba Biblia inamwakilisha Bwana na kwamba imani katika Bwana ni imani katika Biblia. Je, Biblia nzima kweli imetolewa kwa msukumo wa Mungu?

11/02/2018

Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Kufunua Ukweli wa Maelezo ya Viongozi wa Kidini ya Biblia


Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Kufunua Ukweli wa Maelezo ya Viongozi wa Kidini ya Biblia

Wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini mara nyingi huelezea Biblia kwa watu na kuwafanya washikilie Biblia. Kwa kufanya hivi, je, kwa kweli wanamwinua Bwana na kutoa ushahidi kwa ajili Yake? Watu wengi hawawezi kufahanu hili.

10/27/2018

Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Mtu Anaweza Kuokolewa kwa Kumwamini Bwana Katika Dini?


Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Mtu Anaweza Kuokolewa kwa Kumwamini Bwana Katika Dini?

Ndani ya dini, kuna watu wengi ambao wanaamini kwamba, ingawa wachungaji na wazee wanashikilia mamlaka katika ulimwengu wa dini na kutembea njia ya Mafarisayo wafiki, ingawa wanakubali na kuwafuata wachungaji na wazee, wanaamini katika Bwana Yesu, si katika wachungaji na wazee, hivyo basi inawezaje kusemwa kuwa njia wanayoyotembea pia ni ile ya Mafarisayo?

10/24/2018

“Kupita Katika Mtego” – Jinsi Mungu Anavyomwokoa Mwanadamu Kutoka kwa Ushawishi wa Shetani | Clip 5


“Kupita Katika Mtego” – Jinsi Mungu “Kupita Katika Mtego” – Jinsi Mungu Anavyomwokoa Mwanadamu Kutoka kwa Ushawishi wa Shetani | Clip 5

Biblia inasema, "Kwa maana muda umekuja ambao lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu..." (1 Petro 4:17). Katika siku za mwisho, Mwenyezi Mungu anaonyesha ukweli wote unaomtakasa na kumwokoa mwanadamu na Anatuonyesha tabia Yake yenye haki, uadhama na isiyokosewa. Kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho imefanywa kumwokoa mwanadamu ili aweze kujinasua kutoka kwa ushawishi wa Shetani na kurudi kwa Mungu.

10/18/2018

Filamu za Kikristo "Toka Nje ya Biblia" (2) - Je, Tunaweza Kupata Uzima wa Milele kwa Kushikilia Biblia?


"Toka Nje ya Biblia" (2) - Je, Tunaweza Kupata Uzima wa Milele kwa Kushikilia Biblia?

Katika siku za mwisho Mwenyezi Mungu anafanya kazi yake ya hukumu na kuleta njia ya uzima wa milele, na ni kwa kukubali ukweli uliolezewa na Kristo siku zile za mwisho tunaweza kupata uzima wa milele. Hata hivyo wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini wanasema kwamba uzima upo katika Biblia, na ilimradi tu tuzingatie Biblia basi tunaweza pata uzima wa milele.

10/08/2018

“Toka Nje ya Biblia” – Mungu Hufanya Kazi Kulingana na Biblia? | Filamu za Kikristo (Movie Clip 1/2)


“Toka Nje ya Biblia” – Mungu Hufanya Kazi Kulingana na Biblia? | Filamu za Kikristo (Movie Clip 1/2)

Wakati Bwana Yesu alkuwa akifanya kazi Yake katika Enzi ya Neema, akihubiri kwamba ufalme wa mbinguni umekaribia na kuwaleta watu katika njia ya toba, Mafarisayo Wayahudi walimhukumu Yeye, wakisema kwamba maneno na kazi Yake zilikuwa kinyume na sheria za Agano la Kale, eti kuwa zilienda zaidi ya Agano la Kale, na kuwa yalikuwa ni uzushi.

9/12/2018

“Kubisha Hodi Mlangoni” (5) - Bwana Anabisha Mlangoni: Unaweza Kuitambua Sauti ya Bwana (2)


“Kubisha Hodi Mlangoni” (5) - Bwana Anabisha Mlangoni: Unaweza Kuitambua Sauti ya Bwana (2)

Bwana Yesu alisema, "Kondoo wangu huisikia sauti yangu" (Yohana 10:27). Kwa dhahiri, Bwana ananena ili kuwatafuta kondoo Wake wakati wa kurudi Kwake. Jambo la muhimu zaidi kwa Wakristo kufanya wanaposubiri kuja kwa Bwana ni kutafuta kusikia sauti ya Bwana. Mtu anawezaje kuitambua sauti ya Bwana, hata hivyo?

9/09/2018

"Kubisha Hodi Mlangoni" (4) - Bwana Anabisha Mlangoni: Unaweza Kuitambua Sauti ya Bwana (1)


"Kubisha Hodi Mlangoni" (4) - Bwana Anabisha Mlangoni: Unaweza Kuitambua Sauti ya Bwana (1)

Bwana Yesu alisema, "Kondoo wangu huisikia sauti yangu" (Yohana 10:27). Kwa dhahiri, Bwana ananena ili kuwatafuta kondoo Wake wakati wa kurudi Kwake. Jambo la muhimu zaidi kwa Wakristo kufanya wanaposubiri kuja kwa Bwana ni kutafuta kusikia sauti ya Bwana. Mtu anawezaje kuitambua sauti ya Bwana, hata hivyo? Kuna tofauti gani kati ya sauti ya Mungu na sauti ya wanadamu?

9/06/2018

"Kubisha Hodi Mlangoni" (3) - Wakristo Wameamka Baada ya Kumsikia Bwana Akizungumza Wakati wa Kurudi Kwake


"Kubisha Hodi Mlangoni" (3) - Wakristo Wameamka Baada ya Kumsikia Bwana Akizungumza Wakati wa Kurudi Kwake

Bwana Yesu alisema, "Tazama, nasimama mlangoni, na kubisha: mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja na yeye, na yeye pamoja na mimi" (Ufunuo 3:20). Kwa miaka hii yote, Kanisa la Mwenyezi Mungu limeshuhudia kwa uthabiti kuwa Bwana Yesu amerudi, na kwamba amesema maneno ya kufanya kazi ya hukumu ya siku za mwisho.

9/02/2018

"Kubisha Hodi Mlangoni" (2) - Ni Makosa Gani Ambayo Hufanyika kwa Urahisi Zaidi Katika Kumkaribisha Bwana


"Kubisha Hodi Mlangoni" (2) - Ni Makosa Gani Ambayo Hufanyika kwa Urahisi Zaidi Katika Kumkaribisha Bwana

Watu wengi wa imani katika jamii za kidini wanaamini kile wachungaji na wazee wa kanisa wanachokisema, "Maneno na kazi zote za Mungu ziko katika Biblia. Haiwezekani kwa maneno yoyote ya Mungu kuonekana nje ya Biblia." Je, kuna msingi wa kibiblia wa dai hili, hata hivyo? Je, Bwana Yesu aliyasema maneno haya? Katika Ufunuo, imetabiriwa mara nyingi, "Yeye aliye na sikio, na asikie lile Roho anayaambia makanisa."

8/29/2018

"Kubisha Hodi Mlangoni" (1) - Ni Desturi Gani Muhimu Zaidi ya Kuukaribisha Ujio wa Bwana


"Kubisha Hodi Mlangoni" (1) - Ni Desturi Gani Muhimu Zaidi ya Kuukaribisha Ujio wa Bwana

Bwana Yesu alisema, "Kondoo wangu huisikia sauti yangu, na mimi Ninawajua, nao hunifuata" (Yohana 10:27). Pia imetabiriwa mara nyingi katika Ufunuo, "Yeye aliye na sikio, na asikie lile Roho anayaambia makanisa." Sauti na maneno ya Roho ni sauti ya Bwana, na ni kondoo wa Mungu mbao watatambua sauti ya Mungu. Ni tendo gani, basi, lililo muhimu kwa Wakristo wanapoukaribisha ujio wa Bwana?

7/20/2018

“Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari” (3) - Kufichua Fumbo la Kupata Mwili


“Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari” (3) - Kufichua Fumbo la Kupata Mwili

Ingawa watu wanaomwamini Bwana wote wanajua kwamba Bwana Yesu ni Mungu aliyepata mwili, hata hivyo hakuna kweli anayeweza kuelewa ukweli wa kupata mwili. Imetabiriwa katika Biblia kwamba Bwana atakuja tena katika mwili kuzungumza na kufanya kazi katika siku za mwisho. Kama hatumjui Mungu mwenye mwili, basi hatuna namna ya kukaribisha kuja kwa mara ya pili kwa Bwana.

7/17/2018

"Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari" (2) - Je, Kuna Msingi Katika Biblia wa Kurudi kwa Bwana Kupitia Kupata Mwili?


"Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari" (2) - Je, Kuna Msingi Katika Biblia wa Kurudi kwa Bwana Kupitia Kupata Mwili?

Watu wengi katika kukaribisha kuja kwa mara ya pili kwa Bwana wanaweka umuhimu tu katika unabii ulio katika Maandiko kwamba Bwana atashuka kutoka mawinguni kuja tena huku wakipuuza unabii kwamba kuja kwa pili kwa Bwana ni kupitia kupata mwili. Wanatangaza kuwa ya uongo njia yoyote ambayo inashuhudia kuja kwa mara ya pili kwa Bwana kama Mungu kuwa mwili.

7/13/2018

"Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari" (1) - Umeme wa Mashariki Laitikisa Dunia ya Kidini


"Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari" (1) - Umeme wa Mashariki Laitikisa Dunia ya Kidini

Umeme wa Mashariki—kuonekana na kazi ya Mungu katika siku za mwisho limetikisa makundi na madhehebu yote, na kila aina ya wanadamu wamefichuliwa. Kondoo wengi wazuri katika kanisa wangependelea kuteseka kukamatwa kusikodhibitiwa na kuteswa na Chama cha Kikomunisti cha China ili tu kutafuta na kuchunguza Umeme wa Mashariki.